Diamond Platnumz Davido, na Cassper Nyovest, kutumbuiza kwenye uzinduzi wa Big Brother,kesho Jumapili

Diamond , Davido na rapper anayetamba kwa sasa Afrika Kusini Cassper Nyovest wametangazwa kutumbuiza kwenye ufunguzi wa shindano la Big Brother Afrika, Jumapili hii.


Ufunguzi huo utarushwa live kuanzia saa 2 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.

Cassper Nyovest anajulikana kwa ngoma zake kama “Gusheshe” na “Doc Shebeleza” na amewahi kushare jukwaa na wasanii mbalimbali wakiwemo Kendrick Lamar na Wiz Khalifa.

Wengine ni pamoja Dj Dimplez, AB Crazy na Emmy Gee ambao wanafahamika kwa wimbo wao “Rands and Naira”
Previous Post Next Post