Coke Studio yamkutanisha Diamond Platnumz na Yemi Alade, Kuna kitu kizuri kinafuata!

Diamond amekutana na mkali wa Johnny toka Nigeria, Yemi Alade wakati wa kureko msimu wa pili wa Coke Studio.

Wawili hao wanatarajia kurekodi kama pair ya muziki kwa ajili ya kipindi hicho ambacho huwakutanisha wasanii wengi wakubwa Afrika na kufanya muziki kwa pamoja huku wakiimba LIVE. Huenda kukawa na project kati yao siku za usoni.


#wonderment! With the infamous ubertalented six-abbs superstar Diamond @diamondplatnumz #iAmHumbled #thankYouCokeStudio, ForThe Opportunity God bless AFrica.. #cokeastudioafrica @cokestudioafrica @dresomes Nosa @chocolatecity Diamond has been singing your song all morning @audumaikori.” Ameandika Yemi kwenye Instagram na kupost picha akiwa na Diamond.



Naye Diamond alipost picha kwenye instagram wakiwa wawili na kuandika, “Na dem ake Johny @yemialade , ushaelewa nini kinaendelea si eti????.. (jus me and Johny’s Girlfriend….You allready know what it is ryt???....Cc @yemialade.”

Wengine walitengeneza pair katika kipindi hicho ni Vannessa Mdee na Burna Boy (Nigeria), Joh Makini na Chidinma (Nigeria), na Shaa na Jacky Chandiru (Uganda).
Previous Post Next Post

Popular Items

WAKUU WA USALAMA KUHOJIWA KENYA