Ndoa ya Jay Z na Beyonce yawa matatani tena, huu ndio mkasa uliotokea

Drama ya talaka ya Jay Z na Beyonce imeingia hatua mpya kutokana na ripoti kuwa Bey aliwafukuza mashabiki wa kike walioingia kwenye chumba cha kubadilishia nguo cha mume wake wakati wa ziara yao, On The Run.


Beyonce na Jay Z wanaendelea na ziara hiyo lakini tetesi za uwezekano kwa kuwepo wa talaka yao zimeendelea kushika kasi. Vyanzo vimesema kuwa uchepukaji wa Jay Z umemvunja moyo mkewe na hivyo kuna uwezekano mkubwa wakaachana.

Ripoti mpya kutoka jarida la Star inadai kuwa mashaka kati ya wanandoa hayo ni mengi. Jarida hili limevinukuu vyanzo vilivyosema: Jay alikuwa amezungukwa na wasichana wengi chumbani mwake na Beyonce akawafukuza.” Limesema vyanzo vimedai kuwa wanandoa hao wanatumia vyumba tofauti vya kuvalia japo vipo jirani.


Kuna tetesi kuwa Jay Z amewahi kuwa na uhusiano na Rihanna, Rita Ora na kwamba amekuwa na uhusiano wa kimapenzi wa muda mrefu na muimbaji wa R&B, Mya ambaye hata hivyo amekanusha.

Kutokana na ripoti za mumewe kumsaliti, inadaiwa kuwa Beyonce anafikiria kutaka pewa talaka yake.

“She’s heard all the rumors about Jay fooling around, and she can’t take it anymore. The romance is over. He was toasting champagne with the crew and friends and some women who were brought back stage. Beyonce seethed when she saw a busty blonde nuzzling into Jay’s chest and him whispering something into her ear,” limeandika jarida la Star.
Previous Post Next Post

Popular Items