Video: Ben Pol afunguka juu ya Mahusiano yake ya kimapenzi na mshindi wa pili wa Miss Tanzania 2013 Latifa na sababu zilizomfanya adumu naye kwa miezi 9

Uhusiano na mshindi wa pili wa Miss Tanzania 2013, Latifa Mohamed wenye miezi tisa sasa, ndio uhusiano mrefu zaidi aliowahi kuwa nao Ben Pol tangu awe staa.



Ben Pol amesema hayo alipokuwa akihojiwa na tovuti ya Bongo5, kuwa mahusiano yake yaliyopita yalishindwa kudumu kwakuwa wasichana wengi walikuwa na matarajio makubwa kutoka kwake kwakuwa yeye ni msanii. “Sasa hivi tuna miezi tisa, nadhani ndio the longest relationship,” amesema Ben kuhusu uhusiano na Latifa.

Mtazame hapa akiongea zaidi...



“Unajua nimekutana na watu wa aina tofauti. Nimekutana na watu ambao labda wanakuwa na expectations kubwa zaidi kuhusu mtu fulani, kwahiyo akiingia kwenye maisha yako labda kuna vitu ambavyo yeye tayari alishapicture, ‘labda Ben Pol tutakuwa tunakula bata every weekend, tunakula bata milioni, tunaenda huku kule everyday. Kwahiyo mtu anaweza akaja kwenye maisha yako akakuta sio mtu wa hivyo, ni staa ndio lakini you don’t go to clubs mara kwa mara, you don’t do this, you don’t do that kama mastaa wengine. Kwahiyo mtu anakuwa disappointed anatoka kwenye maisha yako. Ndio hicho ambacho nimeexperience zaidi kwenye mahusiano yangu yaliyopita.” “Kwahiyo ukipata mtu ambaye akakuelewa hivyo, inatia moyo kidogo.” Ben Pol amesema hata hivyo uhusiano wake na Latifa haujawa rasmi kabisa kwakuwa bado hajaenda kujitambulisha kwao. “Lakini at least naweza kusema nina hatua moja katika tano au katika tatu.”
Previous Post Next Post

Popular Items