Ray C amuomba samahani Zamaradi na kuwashauri Wema na Kajala wamalize tofauti zao

Mwana muziki Ray C ameamua kufunguka na kupitia ukurasa wake wa instagram nakuwashauri wasanii wapendane napia kuwa kitu kimoja na Rey C pia alimuomba samahani mtangazaji wa Clouds Radio na Tv Zamaradi na kuwataka Wema na Kajala kumaliza tofauto zao



“Kiukweli huwa naumia sana ninapoona mastaa tunatumia muda mwingi kulumbana na kugombana kwa mambo ya kipuuzi sana,mastaa wenzetu wa Nigeria wanatushinda kwa mambo mengi sana sababu wao wanashirikiana na kusapotiana katika mambo mengi sana na hata ukiskia wamepishana basi ujue ni kwa ajili ya biashara tu na si vinginevyo!nilichogundua Mimi ni kwamba kumekua na makundi mbalimbali mitandaoni yanayokuza mambo na kusapoti wasanii kulumbana Mara team simba Mara team nyani!naingea kutoka. Moyoni kuwa watanzania tunasifika kwa kuwa na amani na upendo!sasa iweje tena tuishi maisha ya kuchukiana na ugomvi badala ya kuishi kwa amani?najua sisi wasanii tuna mashabiki wengi. Na tunapenda na nnyie mnatupenda kwahiyo mnatakiwa kutupatanisha tunapogombana na si kutushabikia coz mnaposhabikia ugomvvi ndio mnapotufanya tupoteze muda kulumbana badala ya kutumia huo muda kufanya kazi zetu za sanaa kwa bidii tutangaze nchi yetu tunapoteza muda kulumbana,wenzetu wanaigeria wako mbali sana kwa sababu wanasapotiana sana!wasanii tuache bifu za kijinga na tutumie muda mchache tuliopewa na mola kufanya kazi zetu kwa bidii tutangaze nchi yetu ili vizazi vijavyo virithi bidii zetu,na naomba sana mashabiki wote msapoti mazuri tuyafanyayo”




Ray C baadae alindika hivi kuhusu Zamaradi Mketema kama ifuatavyo :


“Love u zama n sorry for everything keep doing wat u do best @zamaradimketema n hey dogo langu @wemasepetu and my friend @new_kajala tusameheane na tupendane na tupige kazi Africa watutambue bana!!!!!!
Previous Post Next Post