Mwana Fa kuachia wimbo mpya aliomshirikisha AliKiba ‘Kiboko Yangu’

Mwanamuziki wa BongoFlava Mwana FA aka Binamu anatarajia kuachia single mpya ‘Kiboko Yangu’, ambayo amemshirikisha Alikiba Ikiwa ni miezi mitano imepita toka aachie ‘Mfalme’.


Binamu ambaye pia anatarajia kupanda kwenye jukwaa la ‘Serengeti Fiesta’ leo (October 18) akiwa na ‘surprises’ kibao, ameiambia Bongo5 kuwa Jumatano ijayo (October 22) single ya ‘Kiboko Yangu’ itakuwa tayari kwenye vituo vya radio.

Kabla hajaachia ‘Mfalme’ May, 2014, Hamis Mwinjuma alikuwa amepanga aanze kutoa ‘Kiboko Yangu’ ambayo ilikuwa tayari imerekodiwa kwenye studio ya MJ Records kabla ya ‘Mfalme’, lakini mipango ilibadilika.
Previous Post Next Post