Gelly asema muziki umebadilika, na yeye abadilika

Staa wa muziki Gelly wa Rhymes, ameweka wazi kuwa kwa sasa katika soko la muziki, yeye akiwa kama msanii mwenye muda katika game ameona mabadiliko makubwa na vipaji vipya vinavyofanya vizuri.



Gelly amesema kuwa kwa sasa muziki Bongo umeenda kimataifa zaidi kulenga soko la Afrika, na hii ndiyo sababu ya ngoma yake mpya aliyoachia wiki hii, Iyolele, kusukwa kwa lengo la kutosheleza soko hili.

Gelly wa Rhymes amesema kuwa, kwa sasa amekuja na mkakati ya kuliteka soko la Afrika kupitia muziki wake na pia video ya kazi zake ambazo kwa upande wake amejikita kuzitengenezea hapa hapa nchini kwa imani kuwa inawezekana kutengeneza kazi ya kiwango cha juu hapa hapa nyumbani endapo mtu atajipanga.
Previous Post Next Post