Picha: Bill gate afanya kufuru ya Pesa, akodi boti hii kwa wiki ni tsh bilioni 8

Zunguka Duniani kote lakini the top tajiri ni mmoja tu naye ndiye Billgate, Yule tajiri namba moja duniani mwenye utajiri unaofikia dola bilioni 79.2 hivyo kutumia shilingi bilioni nane kwa wiki si kitu kinachoweza kumpunguzia chochote Bill Gates.


Katika boti hiyo helikopta zinamchukua Gates kumpeleke nchi kavu kucheza golf na kumrudisha

Na ndio maana Bill Gates yupo mapumzikoni ambayo tunategemea kwa mtu tajiri zaidi duniani ayafanye.





Tajiri huyo amekodi meli binafsi maarufu yacht ambayo analipa dola milioni 5 (zaidi ya shilingi bilioni 8) kwa wiki.

Tazama picha zaidi hapa




Gates yupo kwenye boti hiyo kubwa na mke wake Melinda na watoto wake Rory, Jennifer na Phoebe nchini Italia.

Mwanzilishi huyo wa Microsoft ameamua kupumzika kwa kukodi yacht hiyo iitwayo The Serene yenye ukubwa wa futi 436 inayomilikiwa Yuri Scheffler.
Previous Post Next Post