Video: Msichana anayedaiwa kuisambaratisha ndoa ya Jay Z atoa ngoma akimchana Beyonce ‘Sorry Mrs. Carter’


Umaarufu nao unashida zake! Familia ya Mr and Mrs Carter haiwezi kukaa siku moja ikatulia bila kupata msukosuko. Tangu ugomvi wa kwenye lifti kati ya Jay Z na Solange, familia hiyo imeendelea kutawala vichwa vya habari kwa taarifa za mpasuko katika ndoa yao.


Na sasa rapper aitwaye Liv, ambaye amekuwa akidaiwa na mitandao ya udaku kuwa mchepuko wa Jay Z ameachia video ya akichana kwenye beat ya wimbo wa zamani wa kundi la Outcast ‘Mrs Jackson’ kurekodi wimbo wake alioupa jina ‘Sorry Mrs. Carter’ na kumchana vibaya Beyonce japo anadai hajawahi kuwa na uhusiano na rapper huyo.

Itazame hapa




Hata hivyo Liv anadai kuwa ni Jay ndiye anamtaka hadi sasa akiwa tayari amemuona Beyonce.
Previous Post Next Post

Popular Items

WAKUU WA USALAMA KUHOJIWA KENYA