R. Kelly anadaiwa deni la $ 1Million, Kufunguliwa mashitaka kama asipolilipa

Mfalme wa R&B, R. Kelly anashitakiwa na meneja wake wa zamani, Derrel McDavid kwa kutokamilisha malipo ya kiasi cha pesa walichokubaliana ili kumaliza uhusioano wao wa kibiashara.


Mwimbaji huyo na meneja wake waliachana mwaka 2013 baada ya kufanya kazi pamoja kwa zaidi ya miaka 20 .



McDavid anaeleza kuwa walikubaliana na Kelly kuwa angemlipa kiasi cha $1 million ili kila mmoja afanye mambo yake.

Kwa mujibu wa TMZ, MacDavid anaeleza katika shitaka lake R. Kelly alimlipa kiasi cha $300,000 kama malipo ya awali lakini hakumalizia kiasi kilichobaki hadi leo.

Inaelezwa kuwa, kwa kuwa McDavid alifanya kazi kwa muda mrefu na R. Kelly, anajua siri zake nyingi ikiwa ni pamoja na masuala ya uhususiano wa kimapenzi yaliyoleta mzozo mkubwa hivyo ugomvi wao unaweza kuwa hatari kwa R. Kelly endapo hatamlipa kiasi hicho na kuvuruga zaidi uhusiano wao.
Previous Post Next Post