Maulidi kitenge sasa asaini mkataba na EFM baada ya kufanya kazi miaka 14 Radio One

Mtangazaji mkongwe wa michezo kwenye kituo cha redio cha Radio One Stereo, Maulid Kitenge ameacha kazi na kwenye kituo hicho na kujiunga na kituo kipya cha redio, EFM.

Kitenge akisaini mkatana wa kujiunga na EFM, kushoto ni Mkurugenzi wa Vipindi, Dickson ‘Dizzo’ Ponela
Katika barua yake ya kujiuzulu, Kitenge ambaye amefanya kazi kwenye kituo hicho kinachomilikiwa na kampuni ya IPP kwa zaidi ya muongo mmoja, amedai kuwa anakwenda kufanya shughuli zake binafsi akidai kuwa ‘hali ya maisha imepanda kwa kiasi kubwa sana na mahitaji ya kimaisha yameongezeka gharama, hivyo inanilazimu kutafuta njia mbadala ya kujiingizia kipato kikubwa zaidi.’


Mtangazaji Maulid Kitenge amefanya kazi Radio One kwa miaka 14.

Credit: Mtaa kwa Mtaa

Previous Post Next Post

Popular Items