Audio: Bob Junior akana kurudiana na mkewe, Illa asema anaumia kuwa mbali na mtoto wake

Producer, Muimbaji na rais wa Masharobaro, Bob Junior amekanusha tetesi zilizokuwepo kuwa amerudiana na mke wake.


Akiongea na segment ya Inbox ya kipindi cha New Chapter cha Radio Free Africa, Bob Junior amesema mazoea ya kuwa na mke na kumuona mtoto wake kila siku yanamfanya awe na huzuni kubwa kuwa mbali nao. Junior amesema aliachana na mke wake na hajarudiana naye tena na hana mpango wa kuoa hivi karibuni.

Hivi karibuni kwenye Instagram Bob Junior alipost picha ya mwanae na kuandika:

Namshukuru Mungu kukupata wewe maisha yangu yote nguvu zangu zote Nitapigana hadi kufa ni kwaajili yako my son Rummy Raheem Rummy maisha yako huta jutia kupata baba kama mimi ila amini kilicho tokea……. ukija kukuua ipo siku utajua yote naishi kwenye maumivu mengi juu yako sana na hapa naandika text hii nalia sana kwa kuwa mbali nawewe sikuoni karibu my son ila jua i love u na kama mapenzi kupenda nasema nitakupenda na hata kuja yoyote kuzidi mapenzi yangu kwako mengine sisemi ila jua mwanangu nipo kwenye wakati mgumu wa kuto kuwa karibu na wewe i love u my son ( rummy .”

Sikiliza mahojiano ya Bob Junior kwenye Inbox hapo chini.

Previous Post Next Post