Siri za Vanessa Mdee usizozijua!

Akiwa anahojiwa na jarida moja la huko nchini Kenya Vanessa Mdee, afunguka mengi ambayo hajawahi kuyasema sehemu nyingine yeyote ile, na kwa wengi wanaomfahamu mkali huyu wa anayezidi ku-make headlines na single yake ya “hawajui”, watabaki midomo wazi kwa vile ambavyo walikuwa hawavijui kabisa kuhusu mwanamuziki huyu kutoka Tzee.


-Moja ya mambo ambayo vanessa huwa hafanyi kabisa mbali na kuwa mwanamuziki, mtangazaji na mwanaharakati ni kupika, Vanessa alifunguka na kusema hata akiwa nyumbani kwake ishu nzima ya kupika haimjii akili kabisa. Tofauti na wanawake wengi wa afrika, hii ishu ni moja kati ya vitu vilivyotokea kuwashangaza wapenzi wengi na wadau wanao mzimia Vanessa.

-Siku alipotoa hit single yake ya “hawajui”, Hii ni moja ya single aliyoitoa kwa watu ambao walikuwa hawamkubali hasa baada ya maneno yao kuzidi kusema kuwa Vanessa hakustahili tuzo ya Kilimanjaro Music Awards aliyoipokea na wengine kusema hakuwa teyari kupokea tuzo hiyo, jambo hili lilimhuzunisha sana Vanessa, hii ilimsukuma vanessa kuandika kuhusu watu wale ambao walikuwa hawamkubali(Haters), na kutoa kitu hiki kinachozidi ku-make headlines kila siku.


-Moja ya mabo ambayo yaliwahi kumshangaza yeye mwenyewe vanessa kama mtangazaji, ni siku alipokuwa ameenda kufanya mahojiano na kiongozi Olesegun Obasanjo, alifunguka na kusema kwamba alipokuwa anamuhoji wajukuu wake walikuwa wakicheza, huku wakimpiga makofi babu yao, Vanessa ilimbidi kushangaa kile alichokuwa anashuhudia, hasa ni jinsi gani kiongozi huyu mkubwa kama yeye anayeheshimika kuzidi kupigwa na wajukuu zake, huku akicheza nao.


-Vanessa alifunguka na kusema kuwa umaarufu kama wake unakuja na faida zake mbali na kuwa na vikwazo vingi katika kazi, moja ya faida zake ni kuwa huwa mara nyingi hapangi foleni anapoenda mahali, alizidi kufumguka na kusema siku moja aliwahi kushikwa na polisi barabarani kwa kutofunga mkanda akiwa anaendesha, polisi alivyofika pale Vanessa aka-smile tu na kumuomba msamaha na officer yale akabidi amuachie tu.



mbali na kufunguka kote huko Vanessa anasisitiza kuwa ni vizuri kwa mtu kutokata tamaa katika ndoto zako, kama alivyosema Lupita, siku moja matunda ya ndoto zako zinaweza kuwa kweli. Vanessa ni mmoja ya watu maarufu wacache wenye vipaji vingi, mbali na muziki hujihusisha na utangazaji wa redio, MC katika sherehe mbalimbali kubwa,ukiacha mbali uanamuziki na harakati zake katika jamii zinazohusu kuelimisha jamii juu ya ukimwi na jinsia.


Previous Post Next Post