Hii ndio zawadi iliyotolewa na Dr Dre kwa washindi wa kombe la Dunia 2014, ni kwa kila mchezaji!

Producer, Rapper na mwanzilishi wa Beats Electronics, Dr. Dre ni miongoni mwa mashabiki wa timu ya taifa ya Ujerumani iliyotwaa kombe la FIFA la dunia jana (July 13) nchini Brazil.



Kutokana na ushindi huo wa Ujerumani Dre ameamua kuipongeza timu hiyo kwa zawadi special ya headphones za dhahabu (special edition 24 carat gold dipped Beats Pro headphones). Wachezaji wote 23 watapata headphones kila mmoja pamoja na meneja wao wa 24.

Naomi Campbell ndiye model aliyehusika katika upigaji picha wa kampeni hiyo ya ‘Golden Project’ ya Beats by Dre. Campbell anaonekana katika picha akiwa amevalia nguo ya rangi ya dhahabu, akiwa ameshika mpira wa dhahabu huku amevaa headphone ya dhahabu.




Akizungumzia furaha yake ya kushiriki katika dili hilo la Beats Naomi amesema:
“Working on the ‘Golden’ project with Beats by Dr. Dre was so much fun. The shoot was loud and energetic…I even got to practice my football skills! This was the first time I’ve had the chance to work with the legendary Rankin, so it was a dream shoot. The ‘Golden’ project is the perfect way to celebrate the German victory and I’m glad to be a part of this campaign.”

Beats By Dre nao pia kupitia akaunti yao ya Instagram wameandika:
“A golden finish @gotzemario. Respect to #BastianSchweinsteiger. @IAmNaomiCampbell with your Custom Celebration Gold Pros. #GER”
Previous Post Next Post