Walioshambulia Kenya si Al Shabaab, 'Uhuru Kenyatta'

Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amesema mashambullio yaliyotokea katika mji wa Mpeketoni, Pwani ya Kenya hayakufanywa na kundi la wapiganaji wa Al Shabaab bali ni watu wanaoihujumu Kenya.

Rais Kenyatta ameyasema hao muda mfupi uliopita wakati akilihutubia taifa la Kenya baada ya mashambulio mawili yaliyotokea Mpeketoni juzi na jana.



Rais amewataja pia wanasiasa na baadhi ya maofisa kuhusika katika mashambulio hayo ambapo baadhi yao wameachishwa kazi tayari na watachukuliwa hatua kali ikiwemo kushitakiwa.



Kundi la Al Shabaab lilikiri kuhusika na shambulio la juzi usiku ambapo watu takribani 50 waliuawa.
Previous Post Next Post