Picha:Ujio mpya wa Chid Benz katika Gemu, afanya collabo na Diamond Platnumz, Ay

Kwa muda mrefu mkali wa Ilala, Chid Benz aka Chuma amekuwa kimya kwenye game na mwaka huu ameamua kurudi tena na ujio mpya unaowakutanisha wasanii wa Tanzania wanaoheshimika kwenye level za kimataifa, AY na Diamond Platinumz.



Chid amepiga story na sammisago exclusively na kuuelezea mfumo wa ngoma yake mpya aliyofanya na wakali hao.

Amesema ni ngoma kali yenye verse 3 ambapo yeye anasimama kwenye verse mbili, AY anainyonga verse 1 halafu mtoto wa Tandale, Platinumz amefanya yake kwenye kiitikio na kibwagizo.

Wimbo huo umetayarishwa na producers watatu, Dully Sykes ambaye amefanya mdundo kwa mara ya kwanza halafu mixing na vocal zimekamilishwa na Tud Thomas na Emma The Boy.

Hata hivyo, jina na tarehe za kuachiwa wimbo huo bado hazijakwa wazi.


Chid ameshare picha mpya kwenye Instagram kuashiria ujio wake:














Previous Post Next Post