Picha: Hivi ndivyo mwili wa Mama yake zitto kabwe ulivyoagwa uwanja wa ndege Dar es salaam kuelekea Kigoma kwa Mazishi

Bi Shida ambae ni mama mzazi wa mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe alifariki dunia hospitali Dar es salaam June 1 2014 alikokua amelazwa katika chumba cha uangalizi maalum (ICU)



Tazama picha za kuaga mwili huo wa Marehemu pale Uwanja wa Ndege Jijini Dar es salaam

Zitto kabwe akiwa na Prof Ibrahimu Lipumba wakati wa kuuaga Mwili wa mama yake kipenzi Bi Shida Salumu aliyefariki leo kabla ya kusafirishwa kwenda Kigoma kwa mazishi

Waheshimiwa Wabunge na Baadhi ya Viongozi wakibeba Jeneza lililobeba Mwili wa Marehemu Mama Yake Zitto Kabwe Bi Shida Salum kuingiza kwenye ndege Tayari kwa safari ya kwenda Kigoma Kwenye mazishi

Prof Ibrahimu Lipumba akijadili jambo na Mwezie baada ya kupakia mwili wa marehemu kwenye ndege kuelekea kigoma Kwenye maziko

Ndege Ikiandaliwa Ili kuweza Kuingiza Mwili wa Marehemu Mama yake Zitto Kabwe

Huyu ni Rais wa TASWA Juma Pinto akiwa VIP ya Terminal 1 JKN Airport alipokutana na Cardinal Pengo wakati wa kuaga mwili wa Mama yake Zitto Kabwe
Previous Post Next Post