Haya ndio Majanga na Mapenzi yaliyowahi mtokea Qchief maishani mwake,

Akiwa ni moja ya wasani wa kongwe sana hapa nchini, Qchief aliwahi kutesa kwa ngoma zake kali sana hapa East africa, na baada ya muda alitoweka ghafla kwenye ulimwemgu wa muziki, hata hivyo baada ya kushuka kwake kimuziki bado nyimbo zake zinapendwa hadi leo. Ni moja ya wanamuziki wachache wanaotengeneza nyimbo ambazo zinaweza kukaa miaka na miaka kutokana na ujumbe wake mzuri,ukiachana na muziki, maisha yake nje ya muziki yamekuwa kitendawili, huku kila mmoja hakuwa anajua  kuna nini haswa kinaendelea na mkongwe huyu mkali katika game hili la muziki.


Kilichomtokea baada ya kuachana na mke wake.
Kama ulishawahi kusikia kipindi cha nyuma kuwa Qchief alikuwa mtumiaji wa madawa ya kulevya, hii ilikuwa ni kweli ila sababu ya kuanza kutumia madawa hayo, inasemekana kuwa Didas ndiye aliyesababisha hadi Qchief aanze kutumia madawa hayo.Hata hivyo Didas mwenyewe aliwahi kufunguka na kusema kuwa, Qchief anamchukia hadi hii leo, huku akimlaumu kuwa yeye ndiye aliyesababishwa kujingiza kwake kwenye janga hilo la utumiaji wa madawa ya kulevya.


Kuhusu maisha yake kimahusiano.
Ilikuwa ni jambo la siri sababu aliyekuwa mke wake hakutaka kuweka mambo yao hatharani, ni moja ya jambo ambalo halikuwa linajulikana na wengi, kama ulishawahi kumsikia mdada maarufu anayejishughulisha na enitertainment business, anayemiliki Didas entertainment ndiye aliyekuwa mke wa Qchief .Mwanadada huyo mfanyabiashara mkubwa mwenye makazi yake huko
nchini uingereza hadi hivi sasa, alifunguka na kusema kuwa, haikuwa rahisi kuwa na mapenzi ya mbali sababu muda mwingi, Qchief alikuwa na wivu, pindi aendapo safarini, haswa pale anaposafiri bila kumtarifu mpenzi wake huyo.Baada ya muda wa usiozidi miezi kumi na mbili wakaamua kuwa kila mmoja aende njia yake.

Unajua kwa nini hasikiki akitoka kupiga show za nje?
Ingawa Qchief ni msanii mkongwe sana, imetokea kutosikika sana kwake akisafiri kwenda nje ya nchi kufanya muziki, kama ilivyo kwa msanii mkongwe mwenzie Ali kiba, Aliyekuwa mke wake Didas aliwahi kufunguka na kusema kuwa mbali na jitihada nyingi za kumtafutia Qchief dili za kupiga show nyingi nje ya nchi,toka hapo zamani, haikuweza kuzaa matunda kutokana na
Qchief kutopenda kusafiri, Qchief aliwahi kukiri kuwa Bongo imemkamata ndiyo sababu hapendi kusafiri na kukaa nchi za watu, ni bora akomae hapa hapa Bongo. Inasemekana kuwa Qchief alishawahi kutafutiwa hadi viza ya kwenda kupiga show nje ya nchi, ila mwisho wa siku alichomoa na kukataa kwenda kabisa.
Previous Post Next Post