Rihanna adaiwa kutaka kuishi pamoja na Drake

Rihanna na Drake hawatengani kama kumbikumbi kwa sasa na inasemekana kuwa Rihanna anataka kumshawishi rapper huyo watafute nyumba ya kuishi pamoja.



Chanzo kimoja kimeuambia mtandao wa HollywoodLife.com: ” Angependa pengine siku moja kuona kama wanaweza kuishi pamoja. Lakini Rihanna hataki kulazimisha chochote.” Wapenzi hao wameshajadili suala hilo lakini hawajaamua kama wako tayari kuupeleka uhusiano wao kwenye level nyingine.

Wawili hao mwanzoni walikuwa wamepanga kuwa na uhusiano wa kawaida tu lakini sasa wameonesha kupendana zaidi.
Previous Post Next Post