Nicki Minaj kukomaa na uigizaji filamu

Baada ya mafanikio ya mapema ya filamu aliyoigiza ya ‘The Other Woman’, Nicki Minaj anafikiria kuuchukulia serious uigizaji wa filamu.



Katika filamu hiyo, Nicki ameigiza na Cameron Diaz, Kate Upton na Leslie Mann ambapo uhusika wake ulikuwa mdogo lakini sasa anataka kuigiza kwenye filamu atakayochukua uhusika mkubwa.

Akiongea na MTV News, alisema: Naenda kwenye usaili, na najaribu kutafuta uhusika sahihi na muongozaji sahihi pamoja na waandishi sahihi. Nataka kuwa sehemu ya kitu kuanzia hatua ya mwanzo, nataka uhusika uliotengenezwa kwaajili yangu.”
Previous Post Next Post

Popular Items