Alichosema AY kuhusu jux na video zake.

Baada ya wimbo wa Jux”Uzuri wako” kubaniwa kuingia katika tuzo za hapa Tzee zijulikanazo kama Kilimanjaro Music awards, hata baada ya watu kupendekeza iingie katika kinyang’anyiro cha tuzo hizo, kwa sababu tu video yake ilikuwa haina maadili, imepingwa na msanii mkongwe AY na kusemekana kuwa,


waandaaji wa tuzo hizo inabidi wabadili muonekano wa mambo hivi sasa, sababu kila mtu ana creativity yake na bila shaka zile ni tuzo zinazohusu nyimbo tu, siyo tuzo za video, na ukiachana na hivyo haikustahili kutolewa cause haina hata maneno mabaya ya kimaadili kufanya iweze kutolewa katika tuzo hizo.


Wasanii wengi waliweza kuliongelea hili jambo kwa wakati tofauti na kila mtu kutopata ufafanuzi kwa hilo lilotendeka, sababu kuna video nyingi zinazoendelewa kupigwa hapa nchni ambazo hazina maadili na kuendelea kupigwa kaika media za hapa Tzee, Jux mwenyewe alishangaa kwa nini kufungiwa kwa video yake bila ya upokea maelezo yoyote, na video nyingi kuendelewa kupigwa katika media bila kufungiwa ingawa zina ukali wa mambo kuliko hata video yake.
Previous Post Next Post