Criss Brown Ashitakiwa kwa kumpiga mchezaji wa basketball

Msanii wa R n B Chris Brown ambaye wiki hii ameingia tena kwenye msala mwingine baada ya kushitakiwa kwa kosa la kumpiga mchezaji wa mpira wa kikapu.


Brown ambaye anaendelea kurecover rehab, anadaiwa kumpiga mchezaji huyo aitwaye Malcolm Ausbon katika mechi ya mpira wa kikapu mwezi July mwaka jana (2013), lakini sasa hivi ndio mchezaji huyo ameamua kumfungulia mashitaka.

Mlalamikaji anadai kuwa Chris alimsababishia majeraha sehemu za usoni, kichwani, shingoni mgongoni, miguuni na kwenye mbavu kiasi cha kupelekwa chumba cha dharula, na kuongeza kuwa tukio hilo lilimsababishia aibu, hofu wasaiwasi na stress.

Katika barua ambayo TMZ wameipata, mwanasheria wa Malcom amemwandikia mwanasheria wa Chris kudai fidia ya $250,000 ili kumaliza tatizo hilo.

Malcom amewafungulia mashitaka Breezy na timu yake ya usalama.

Chanzo kimoja kimeiambia TMZ kuwa Chris Brown amekiri kuwepo kwa tukio hilo, lakini amekana hakuna mtu aliyepigwa katika tukio hilo.

Source:Tmz
Previous Post Next Post

Popular Items