Birdman kusheherekea birthday party yake na Models wa Kike Wapatao 730, Kugharimu tsh mill 800

Katika kusherehekea siku yake ya kuzaliwa ya miaka 45, Birdman ataangusha party ya nguvu itakayogharibu dola laki 5 (sawa na shilingi milioni 800) itakayokuwa na walimbwende watakaokuwa watupu, crew yote ya Young Money na gari zake zote zinazofikia thamani ya dola milioni 7.


Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, sherehe hiyo itafanyika Jumamosi usiku katikati ya NBA All-Star Weekend. Rapper huyo amekodi uwanja alioupa jina “Birdman’s New Era Voodoo Lounge.”

Pamoja na wanawake 30 walio watupu, kutakuwa na models wengine 700 watakaovaa nguo. Zaidi ya hapo atasafirisha gari zake kutoka Miami ambazo kwa pamoja zina thamani ya dola milioni 7 zikiwemo Bugatti 2, Maybachs, 2 na basi 3 za tour.

Wageni waalikwa ni pamoja na James Harden, Paul George, Blake Griffin, Shaq, Kenny Smith na rappers wa Young Money, Lil Wayne, Drake, Nicki Minaj, na wengine. Pia wasanii wa zamani wa Cash Money, Mystikal, Turk, Juvenile, na Mannie Fresh watakuwepo.

Previous Post Next Post