Ney wa Mitego Ambembeleza Mpenzi wake baada ya Kuona Video ya Nakula ujana' Ni kweli wewe ndio unastahili kushika hicho kifua laki hizi kazi tu...'

Nay wa Mitego ametoa video mpya ‘Nakula Ujana’ wiki iliyopita ambayo imefanyika nchini Kenya. Katika video hiyo Nay ameonekana akila ujana haswaaa huku akiwa amezungukwa na mabinti wazuri watano wa Kenya, waliojifunga taulo huku wakichezea kifua cha hit maker huyo wa ‘Muziki gani’ ambacho kiko wazi.


Inavyoonekana video hiyo imeleta wivu kwa mpenzi wa Nay hasa kutokana na jinsi alivyojiachia na warembo hao, hali iliyopelekea Nay atumie Instagram kumtoa wasiwasi ‘mrs Nay’ juu ya wasichana hao walioonekana naye kwenye video, hiki ndicho alichokiandika;




Ney wa Mitego aliandika hivi,  “Daaaaah!! #Nakula #ujana #video inataka kuharibu kwa bby… #966 ckiliza mrs nay hii ni video 2 hakuna kingine kilichoendelea baada ya apo,,, ni kweli we ndo unastahili kushika icho kifua bt ni kazi 2 na nikatika kufanya ki2 kizuri.. plzz tusigombane bcoz of zat zic video,, sawa angeweza act m2 mwingine bt ckuona haja yakumuweka m2 nilitakiwa kuonyesha uhalisia kidogo…@wemalious mi penda wewe sana kila m2 anajua,, wale mabinti wa kikenya wackupe presure#966″.
Previous Post Next Post

Popular Items