PICHA: WAPENZI MAPACHA WALIOFUNGA NDOA WAINGIA KWENYE 'GUINESS BOOK OF THE WORLD RECORDS'

Couple mbili za mapacha wanne wanofanana (identical twins) wa Nigeria, wamefanya kile kinachoaminika kuwa ni cha kipekee na cha kwanza kuwahi kufanyika nchini humo, baada ya kufunga ndoa zao siku moja na kufanya sherehe moja.


Mapacha hao wa kiume (Febisola Kehinde Okunniyi na Chibuzor Adelakin Okueze) walifunga ndoa na wapenzi wao mapacha wa kike (Folawemi Taiwo Okunniyi na Chinonso Akinade Okueze) Jumamosi iliyopita (Nov 30) huko Lagos, Nigeria.

Mtandao wa Daily Star wa Nigeria umedai kuwa ndoa za mapacha hao wanne kwa pamoja huenda zikawa za kwanza kwa Afrika, na kwa mujibu wa maafisa wa kitabu cha rekodi za dunia ‘Guinness Book of World Records’, ni ya 251 duniani.


SOURCE: DAILY STAR
Previous Post Next Post