Kajala akana tuhuma za kutembea na Mume wa Shamim Mwasha (Blogger maarufu nchini)

Msanii wa filamu nchini Kajala Masanja amefunguka ya moyoni na kudai kuwa amechoshwa kuzushiwa anatembea na mume wa mmiliki wa blog ya mitindo nchini (8020 Fashions) Shamim Mwasha huku akidai kuwa si kweli.

Baada ya gazeti moja la udaku linalotoka kila jana kutoa taarifa tata juu ya mwigizaji maarufu wa filamu nchini Kajala Masanja kuwa, kwa mdada huyu sasa ameamua 'kuiingilia ndoa ya Shamim Mwasha - blogger na mmiliki wa 8020 fashion boutique, leo hii kupitia mtandao wa kijamii maarufu nchini mwanadada huyu amefunguka kuhusu tuhuma hizo na kujibu haya yafuatayo...


Kajala ameamua kukanusha tetesi hizo kupitia akaunti yake ya Instagram baada magazeti ya udaku kumtuhumu amekuwa akitembea na mume wa Shamim.

“Nadhani namjua huyu dada siku nyingi sana kabla ata ya wengine wenu kumjua tunaheshimiana sna na atujawahi kukoseana sasa sijui nani alie anzisha habari ya mimi natembea na mume wake na sijui alifanya ivyo kwa makusudi gani naumia kila siku kwaajiri ya ujinga wa watu na hayo magazeti nikiwaambia nipeni ushahidi wa kuwa natembea na mume wa shamim sijui kama mtafanya daah sijui nisemeni nini @8020fashions mpz enjoy ndoa yako acha na wapumbavu nimevumilia nimeona bora leo niandike unajua sipendagi kuongea lkn gazeti la jana limenikwaza sana,” aliandika Kajala.
Previous Post Next Post