Kama wewe una kipaji cha kuigiza, kauli hii ya Salma Jabu “Nisha” haitakiwi kukupita

Muigizaji wa filamu mwenye jina kubwa ndani ya bongomovies Salma Jabu Nisha amemwaga chozi la huruma kutokana na jinsi wasanii wachanga wa filamu wanavyohangaika ili watoke huku wakipuuzwa na baadhi ya wasanii wenye majina makubwa. Akizungumza na tovuti ya Swahiliworld planet ,Nisha ameahidi kuendelea kuwasaidia wasanii hao kwa kufanya usaili mara kwa mara pindi anapokaribia kutaka kutengeneza filamu mpya kupitia kampuni yake ya Nisha's Film Production ambayo tayari imeanza kufanya kazi na wasanii wachanga katika filamu yake mpya ambayo ilimalizika shooting hivi karibuni.

Nisha alisema kuwa hata yeye alipitia msoto kama huo kabla ya kuto hivyo anajisikia huruma na industry hii ili izidi kukua ni lazima mastaa wa sasa wawaandae wasanii chipukizi ambao ndiyo watakaotingisha siku za mbele na kuzipeleka filamu za Tanzania katika level za kimataifa. Hii ina maana kuwa baada ya filamu hii mpya ya Nisha kuingia sokoni hivi karibuni atafanya usaili mwingine wa wasanii wachanga amabo atafanya filamun mpya nao. "nawapenda sana wasanii chipukizi nikiwaona huwa nasikia uchungu mpaka machozi hunitoka kwa wanavyohangaika kila siku kutafuta sanaa naahidi kuwasaidia" alisema Nisha

Big Up  sana Nisha kwa hilo. Kazi kwenu wenye vipaji kuanza kumsaka Nisha alipo.


Source:BongoMovies 

Previous Post Next Post

Popular Items