Picha: Sheria Ngowi akutana na bango lenye picha ya Flaviana Matata katika duka la nguo za kike Marekani



Flaviana Matata ni mrembo anayeipeperusha vizuri bendera ya Tanzania nchini Marekani kupitia mafanikio anayozidi kupata kila kukicha katika ulimwengu wa mitindo.


Hii ni picha ambayo mbunifu wa mitindo Sheria Ngowi amepost ikimuonesha akiwa mbele ya duka la nguo na accessories za wanawake linaloitwa Aritzia nchini Marekani likiwa na bango lenye picha ya mwanamitindo wa Tanzania Flaviana Matata.

Kupitia Instagram Sheria alipost picha hiyo na kuandika,

“Look who I just spot in Soho??? @flavianamatata you inspire me to do big things and become greater! Very proud of you!”

Na Flavy aka comment:
“Awwww thank you @iamsheriangowi we will get there God willing
Previous Post Next Post