Kutoka Kwa Obama: Gari la ziara la 2 Chainz lakamatwa na Polisi likiwa na silaha na madawa



Pistol mbili, shotgun moja na dawa za kupunguza maumivu vilipatikana kwenye basi la tour la 2 Chainz mwezi uliopita alipokamatwa na watu wengine 10, kwa mujibu wa nyaraka za mahakamani zilizowasilishwa jana.
Rapper huyo mwenye miaka 35, ambaye jina lake halisi ni Tauheed Epps, alikamatwa August 22 kwenye jiji la Oklahoma City baada ya polisi kusimamisha basi hilo.
Kwenye ukaguzi huo polisi walikamata pia madawa ya hydrocodone na Flexeril ambayo hayakuwa yameelekezwa na daktari. Flexeril hutumika kupoza misuli na hydrocodone hupunguza maumivu. Maofisa pia walikamata mabaki ya bangi na karatasi za kusokotea.
Previous Post Next Post