WAFUASI WA MORSI HAWATAKI KUPATANA



073 3e4c7
Chama cha rais aliyetolewa madarakani, Mohammed Morsi, hakikubali juhudi za kupatanisha zinazofanywa na mmoja kati ya viongozi wakubwa wa kidini nchini Misri. (HM)
Waandamanaji wa Misri
Msemaji wa mashauri ya nchi za nje wa chama cha Bwana Morsi, cha Freedom and Justice Party, aliuliza ikiwa imamu mkuu wa al-Azhar kweli hapendelei upande wowote.
Alisema imamu huyo alipanga njama dhidi ya rais, na aliunga mkono jeshi kumpindua Morsi.
Mohammed Soudan aliongeza kusema kuwa haikuelekea chama chake kuombwa kuzungumza wakati viongozi wake wako jela au wanakabili mashtaka.
Chama hicho ni tawi la siasa la Muslim Brotherhood.
Bwana Soudan piya alionya kuwa maandamano ya wafuasi wa Bwana Morsi yataendelea na kwamba watu wako tayari kufa. 

News Via:  bbcswahili
Previous Post Next Post

Popular Items