Mzee Magali (Bongo Movie) aingia kwenye Bongo Flava, amesharekodi single moja


Kweli mwaka 2013 utakuwa na surprise nyingi sana!! So far tumeshapata surprise kibao ikiwemo ile ya kutoka kwa promoter na Mkurugenzi wa Watanashati Entertainment, Ostaz Juma na Musoma kuingia kwenye hip hop na kurekodi wimbo mmoja aliomshirikisha Young Killa.
71e5bb98eecc11e2972d22000aa82023_7
Zamaradi Mketema akiwa na Mzee Magali
Surprise zinaendelea na sasa inakuja bombshell nyingine. Kwa mujibu wa mtangazaji wa Take One ya Clouds TV, Zamaradi Mketema, muigizaji wa filamu nchini maarufu kama Mzee Magali ametupa karata yake kwenye muziki.
“Mzee magali augeukia mziki wa bongo fleva now.. sikiliza movie Leo siku ya KESHO on CLOUDS FM Radio ili usikie wimbo wake mpya kabisa wa kwanza ambao ameufanya SAA NNE name Dk 45 asubuhi,” ameandika Zamaradi kwenye Instagram.
Unahisi Mzee Magali anaweza kueleweka kwenye muziki? Funguka.
Previous Post Next Post