RAISI JAKAYA KIKWETE ATUA NCHINI SINGAPORE KWA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU 3! AKUTANA NA WAFANYABIASHARA ZA UJENZI WA NCHINI SINGAPORE


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Bw. Laurence Bay, Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Singapore. Kushoto ni Balozi wa Tanzania India na Singapre Injinia John Kijazi na mbele yao ni Naibu Mkurugenzi wa Itifaki wa Singapore Bi. Christine Tay.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Mh. Bernard Membe,akifuatiwa na Waziri wa Viwanda na Biashara,Mh. Abdallah Kigoda pamoja na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi,Mh. Anne Tibaijuka wakati Rais akiwasili nchini Singapore jana
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mbunge wa Kasulu mjini Mhe Moses Machali pamoja na wadau wengine wakati akiwasili Singapore.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea jijini Singapore jana wakati alipokutana na wafanyabiashara za ujenzi wa nchi hiyo mara tu baada ya kutua kutoka Japan alikokuweko kwa ziara ingine ya kikazi. Katika mkutano huu Rais Kikwete aliwakaribisha wafanyabishara hao wa Singapore Tanzania kuwekeza katika sekta ya nyumba wakati wa chakula cha jioni kilichiandaliwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).

Picha na IKULU
Previous Post Next Post

Popular Items