KAMATI KUU CHADEMA KUKUTANA DAR


8 e3b83
                                TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 
 
KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) itakutana kwa siku mbili kwenye kikao chake cha kawaida jijini Dar es Salaam, kuanzia tarehe 3-4 Aprili, 2013.
 
Katika kikao hicho cha siku mbili, Kamati Kuu itajadili pamoja na mambo mengine, yatokanayo na kikao kilichopita, hali ya kisiasa nchini, pia itapokea taarifa ya utekelezaji wa maazimio ya kikao cha Baraza Kuu kilichofanyika mwezi Februari mwaka huu, ikiwemo mpango wa uendeshaji chama kwa kanda.
 
Aidha, Kamati Kuu pia itajadili mpango kazi na bajeti ya Chama kwa mwaka 2013-2014
 
 
Imetolewa Aprili 2, 2013, Dar es Salaam na;
 
Tumaini Makene
Ofisa Mwandamizi wa Habari CHADEMA
Previous Post Next Post

Popular Items