BREAKING NEWS: BI. KIDUDE AFARIKI DUNIA


Mwanamuziki gwiji nchini Fatuma Binti Baraka "Bi Kidude" hatunaye tena. Taarifa toka kwa familia yake zinasema Bi Kidude aliekuwa akipatiwa matibabu katika hospitali ya Hindu Mandal amefariki leo. Bi Kidude atakumbukwa kama mwanamuziki mkongwe zaidi nchini ambaye alianza muziki akiwa na umri wa miaka 10 tu na aliwahi kupokea tuzo mbalimbali kutokana na mchango wake katika muziki wa mahadhi ya mwambao. Hakika sanaa nchini imepoteza moja ya nguzo kubwa.

Pumzika kwa amani Fatuma Binti Baraka.

Previous Post Next Post