
Askari wa Jeshi la wananchi wakiwa katika operesheni ya kuokoa majeruhi na kutafuta miili ya watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo huko Moshono mkoani Arusha (Picha kwa hisani ya Mtandao wa Grobalpublishers).
……………………………………………………………..
Na Gladness Mushi wa Fullshangwe-Arusha 
Zaidi ya wachimbaji 25  wa moramu wanasadikiwa kufa huku  watu zaidi ya sasa  14 wakiwa wamepoteza maisha kutokana na kuagukiwa na kifusi” wakati wakiwa kwenye shuguli zao  za uchimbaji mawe ya moramu katika eneo la Moshono jijini
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo wamesema kuwa lilitokea asubuhi ya leo kati ya saa nne na saa tano za asubui ambapo vijana hao walishuka katika mgodi huo kwa malengo ya kuchimba Moramu
Tukio hilo  lilitokea kati  ya saa nne na  saa tano za asubuhi mara baada ya mgodi huo kujaa maji kutokana  na mvua kubwa ambazo zinanyesha mkoani Arusha  hali ambayo ilisababisha mawe ya migodini kushuka  ndani ya mgodi huo ukiwa na wachimbaji pamoja na madereva wa magari ya kubebea moramu hizo
Mvua  kubwa ikiwa inaendelea kunyesha baadhi ya watu waliokuwa juu ya mgodi huo waliona kimya kimezidi kwa muda mrefu sana kwa kuwa sio kawaida ya wachimbaji wa mgodi huo kukaa muda mrefu bila shughuli zozote kuendelea mgondini hapo.
Ilibidi wasogee  katika mgodi  huo ambapo  giza kubwa ambalo liliwatatanisha sana hali ambayo iliwafanya wapigiane simu na kukusanyika katika eneo hilo ambapo walianza uchunguzi na kugundua kuwa kifusi  kubwa sana kilikuwa kimeshkuka katika mgodi huo na kufukia wachuimbaji hao.