
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Hamis Sadifa

Vijana machacahari Mtela Mwampamba na Juliana Shonza walioihama Chadema hivi karibubi, wakiserebuka nje ya Ofisi ya CCM mkoa wa Morogoro, baada ya msafara wa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Taifa, Sadifa Hamis Juma kuwasili kwenye ofisi hiyo, Februari 28, 2013 kuanza ziara ya siku tatu mkoani humo.

Sadifa akipatiwa burudani ya shairi na mmoja wa waghani maarufu wa mashairi mkoani Morogoro.Kulia ni Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro, Sixtus Mapunda

Mwenyekiti wa UVCCM, Sadifa Hamis Juma akiwa na Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro, Sixtus Mapunda wakati wa mkutano wa ndani kati ya Mwenyekiti huyo na wajumbe wa Baraza la Vijana mkoa wa Morogoro

Mkuu wa Utawala wa UVCCM Taifa, Abdallah Mpokwa akitoa utambulisho wa watu walioambatana na Sadifa kwenye msafara huo, katika ukumbi wa CCM mkoa wa Morogoro

Kada wa CCM aliyehamia kutoka Chadema hivi karibuni, Mtela Mwampamba akisalimia baada ya kutambulishwa ukumbini.

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mjini Magharibi, Zanzibar, Juma Borafya akisalimia baada ya kutambulishwa kwenye kikao hicho cha ndani. Wapili kulia ni Katibu wa CCM Wilaya ya Morogoro mjini, Ali Issa, Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM, Taifa, Mfaume Kizigo na Sixtus Mapunda

VIVA VIJANA VIVAAAA!!!!!, Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro Sixtus Mapunda akiongoza salaam maalum kwa Vijana wa UVCCM ukumbini. Pamoja naye kutoka kulia ni Katibu wa CCM Morogoro, Ali Issa na Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM Mfaume Kizigo. Walioketi kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Morogoro Harrieth Sutta na Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Sadifa.

VIVAAAA!!!, vijana wakiitikia salam ya Sixtus ukumbini, baadhi yao ni Shonza na Abubakar Assenga

VIVAAAA, VIVAAAA!!!!, Vijana wakiitikia salam

Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Morogoro Herieth Sutta akimkaribisha Sadifa kuzungumza kwenye mkutano huo. Kulia ni Sixtrus Mapunda

NAFURAHI KUWA NA WEWE! Sadifa akimwambia Sixtus Mapunda kabla ya kuanza hotuba yake ya mkutano huo wa ndani uliofanyika Ofisi ya CCM mkoa wa Morogoro

Sadifa akizungumza kwenye mkutano huo wa ndani

Sadifa akisisitiza jambo

Na kusisitiza zaidi

Sadifa akizidi kusisitiza hotuba yake huku viongozi wakiwa makini kumzikiliza

ULIOCHAGULIWA MSIJIKWEZE, JISHUSHENI KWA WANACHAMA", Anasema Sadifa

"Wapendeni waliowapinga wakati wa uchaguzi" msiwanunie, kama mtu hakukuunga mkono leo kwa hili ipo siku atakuunga kwa jengine", akasema
Sadifa akitoka na wenyeji wake ukumbini