HAWA NDIO BILLIONAIRES WA5 WA DUNIA AMBAO WANA UMRI MDOGO ZAIDI

Namba 1  ni Dustin Moskovitz
Dustin Moskovitz
Umri: 28
Thamani ya utajiri wake: $13.8 billion
WASIFU WAKE: Aliwahi kuishi chumba kimoja na Mark Zuckerberg, Alikuwa moja ya wafanyakazi kampuni ya Facebook ambayo ana mchango mkubwa katika kuanzishwa kwake, Hadi sasa Moskovitz huwa anatumia usafiri wa baisikeli kwenda kazini. Anapanda ndege za wananchi wa kawaida anaposafiri.

Namba 2 ni Mark Zuckerberg
Mark Zuckerberg
Umri: 28
Thamani ya utajiri wake: $13.3 billion
WASIFU WAKE: Ndio mwanzilishi wa Mtandao wa kijamii maarufu wa Facebook ambao ndio chanzo kikuu cha utajiri wake.


Namba 3 ni Albert von Thurn und Taxis
Albert von Thurn und Taxis
Umri: 29
Thamani ya utajiri wake: $1.5 billion
WASIFU WAKE: Jina lake liliingia katika orodha ya Matajiri inayoandaliwa na Forbes akiwa na umri wa miaka 8, lakini alirithi rasmi utajiri aliokuwa nao mwaka 2001 alipotimiza miaka 18, Ni mpenzi mkubwa wa Rally za magari, Yeye pia hushiriki mbio mbalimbali za magari huko Ujerumani.


Namba 4 ni Scott Duncan
Scott Duncan
Umri: 30
Thamani ya utajiri wake: $5.1 billion
Duncan ni mtoto wa mwisho wa Dan Duncan - Billionea aliyepata utajiri mkubwa kutokana na biashara ya gesi kupitia kampuni ya Enterprise Products Partners ambayo mpaka sasa inamiliki eneo lenye ukubwa wa maili 50,000 zenye gesi asilia na mafuta.

Namba 5: Eduardo Saverin
Eduardo Saverin
Age: 30
Thamani ya utajiri wake: $2.2 billion
Ni moja ya waanzilishi wa Facebook pia, Alijivua uraia wa Marekani mwaka 2011, na alishawahi kuingia katika vita kali ya maslahi na Facebook na kutulia baada ya kupewa asilimia 5 za shares, Kwa sasa anaishi huko Singapore ambapo anaendesha biashara zake nyingine. 

#JFYI: Thamani ya utajiri ni kwa dola na imezingatia fedha zao ambazo hazipo katika mzunguko tu
Previous Post Next Post

Popular Items

WAKUU WA USALAMA KUHOJIWA KENYA