Dawa za kulevya zilizomuingiza Chidi Benz kwenye msala thamani yake haizidi hata elfu 50

Chidi Benz tayari yuko uraiani toka asubuhi ya leo ikiwa ni siku tano toka alipokamatwa kwenye uwanja wa ndege wa Julius Nyerere siku ya Ijumaa (Oct.24), na kuwa chini ya polisi hadi alipoachiwa kwa dhamani leo (Oct 29).



Kete 14 za Heroine alizokamatwa nazo Rashid zilikuwa ni gram 0.85 ambazo thamani yake ni shilingi 38,000 pamoja na misokoto miwili ya bangi yenye thamani ya shilingi 1,000 kwa mujibu wa 255 ya XXL ya Clouds Fm.

Rashid Makwiro a.k.a Chidi Benz ametoka baada ya kutimiza masharti ya dhamana ambayo ni shilingi milioni moja pamoja na wadhamini wawili, na kesi yake itasikilizwa tena November 11,2014.
Previous Post Next Post

Popular Items