Mbinu alizotoa Ay kwa wachezaji wa Bongo kuweza kupata nafasi klabu kubwa duniani

Msanii wa Bongo Flava, Ambwene Yesaya ametoa mbinu mpya na rahisi kwa wachezaji nchini Tanzania kutumia teknolojia ya mtandao kujitangaza kimataifa.

Akiongea katika kipindi cha Maskani cha 100.5 Times Fm wakati wakifanya mjadala wa michezo na Gardner Habash na Clifford Mario Ndimbo, AY aliwashauri wachezaji wa Tanzania kuhakikisha wanaweka vipande vya video za mechi au sehemu walizocheza vizuri zaidi ili kujipa nafasi ya kuangaliwa na dunia nzima.



Alieleza kuwa ligi za hapa nyumbani ni vigumu kuangaliwa na wadau wakubwa wa mpira duniani lakini kwa kutumia channel za Youtube ni rahisi watu hao kuangalia video zao hata baada ya muda mrefu kupita na wanaweza kuvutiwa na uchezaji wao.

Aliongeza kuwa aliwahi kuzungumza na rafiki yake mmoja kutoka Uingereza ambaye ana nafasi katika timu ya Manchester United na akajaribu kumdadisi kama wanaweza kufanya mpango wa kuona vipaji vya wachezaji kutoka Tanzania lakini swali moja tu lilikuwa jibu tosha.

“Aliniuliza ‘kuna channel za YouTube za wachezaji wa Tanzania ambazo tunaweza kuona kazi zao?.”

chanzo:TimesFm
Previous Post Next Post