Hiki nicho kiatu cha gharama kubwa zaidi duniani, alichovaa Nick Cannon bei yake iko hapa

Mchekeshaji Nick Cannon amethubutu kuonesha jeuri ya pesa baada ya kuvaa kiatu chenye gharama kubwa zaidi duniani na kupanda nacho kwenye jukwaa la fainali za shindano la American Got Talent.

Nick alijisahaulisha matatizo ya ndoa yake na mwimbaji Mariah Carey mwenye utajiri wa zaidi ya $510 Million na hakusita kukionesha wakati anapigwa picha na kukiweka kwenye mtandao.

<


Kiatu hicho kilichoonekana kuwa na mng’ao wa aina yake ikiwa na mchanganyiko wa rangi zenye almasi na dhahabu, kinauzwa $2.2 Million.

Kuonekana jukwaani na kiatu hicho iilikuwa ndoto ya Cannon tangu mwaka jana alipomfuata sonara maarufu aliyekiunda kiatu hicho, Jason Arasheben na kumweleza mpango wake.



“'Not very often do I get a request for the most expensive shoes in the world. When Nick approached me last year, he said he wanted to make history and be so over the top.” Ameeleza sonara huyo.

Nick alikitendea haki kiatu hicho kwa kutupia saa ya gharama aina ya Rolex na suti za maana.
Previous Post Next Post