Barack Obama amempigia simu waziri mkuu wa Israel Kuhusu vita ya Gaza

Vita kati ya Israel na Palestina inayoendelea inazidi kuwaumiza zaidi wanawake na watoto hasa wa Palestina kufuatia mashambulizi makali yanayoendelea.

Rais wa Marekani, Barack Obama amempigia simu waziri mkuu wa Israel, Benyamini Nyetanyahu jana usiku akimuomba atoe amri ya kusitisha mashambulizi bila masharti.




Kwa mujibu The Times, simu hiyo ya Barack Obama kwa Nyetanyahu inakuja wakati ambapo Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa likitoa wito na kutafuta muafaka wa kusitisha mapigano bila masharti kwa pande zote mbili katika ukanda wa Gaza.

Zaidi ya watu 1000 raia wa Palestina wameua huku askari 21 wa Israele wakiripotiwa kuuawa kutokana na mashambulizi wa Hamas.

Palestina inaathirika zaidi na vita hiyo, kitu kilichompelekea waziri wa mambo ya nje wa Tanzania, Benard Membe kufanisha na mtu anayetumia manati mbele ya mtu malipizi kwa kutumia makombora.
Previous Post Next Post