Nikki wa Pili ' Niliwahi kuuza sambusa darasa la 3 mpaka la 7' haikuwa Raisi, msikilize hapa

Kama jisi Drake alivyoimba katika wimbo wake ‘We started from the Bottom’ lakini Mweusi Nick wa Pili anasema ‘Haikuwa Rahisi’.

Nick wa Pili ambaye ni moja kati ya rappers bora zaidi Tanzania na mshindi wa tuzo ya KTMA ameelezea jinsi alivyohangaika wakati akiwa shule ya msingi katika maisha ya kawaida ambayo wapo watanzania wengi wanayoyaishi hadi hivi sasa.




Akizungumza katika kipindi cha The Jump Off ambapo yeye ndiye Mkali wa The Jump Off wa Wiki hii anayesimulia story ya maisha yake ambayo ni somo tosha kwa vijana ambao wanahangaika kutafuta, rapper huyo ameeleza jinsi alivyofanya shughuli ya kuuza sambusa akiwa darasa la tatu hadi darasa la saba kila anapotoka shuleni saa nne usiku huku akiwasaka wateja kokote walipo..

“Mimi maisha yangu niliyopitia unajua sio kama watu wanavyonidhania, mimi nimepitia a very hard life. Mimi kuanzia nikiwa darasa la tatu nilikuwa nauza sambusa. Nilikuwa natembeza kwenye nyumba za gongo, banana, mabaa na nilikuwa nauza kuanzia saa kumi hadi saa nne usiku, niko darasa la tatu nimeuza mpaka darasa la saba. Kwa hiyo watu wanapotuona Nick wa Pili… it’s not easy. Nafikiri kama ukipata kusikiliza albam ya Chindo kuna ngoma inaitwa ‘Haikuwa Rahisi’ nilijaribu kuweka historia yangu pale..ilikuwa ngumu.”

Nick wa Pili ambaye ni mdogo wake Joh Makini, ameeleza kuwa hata alipomaliza darasa la saba kuingia sekondari ilikuwa ngumu kutokana na kikwazo cha fedha.

Ilimbidi akae nyumbani miezi miwili akitafuta shilingi 20,000 za karo. Bahati nzuri rapper huyo alizipata fedha hizo na alipoingia shule alikuta tangazo la mtihani wa kumaliza muhula na alipoufanya alishika nafasi ya pili kutoka mwisho.

Kutokata tamaa na kukaza ndiko kumempa nafasi ya kung’aa na kupata shahada ya uzamili (masters) na kufanya vizuri kwenye muziki hadi sasa.

“Kwa hiyo ndio life tuliyopitia, lakini if you put a struggle in everything…it’s possible.”

Nick ameachia wimbo wake mpya alioupa jina la ‘Staki Kazi’ akiwa amewashirikisha G-Nako na Ben Pol.

Msikilize hapa


Previous Post Next Post