Samsung Galaxy S5 yaingia sokoni rasmi

Simu mpya ya Samsung Galaxy S5 jana Ijumaa iliingia sokoni rasmi .baada ya sumsung s4 kuwepo sokoni kwa muda hivi sasa.



Mbali na Sumsung kutoa rasmi S5 kumekuwepo na mitazamo ya kutofautiana kuhusiana na simu hizi ambapo wachambuzi wengine wa masuala ya simu, wanadai S5 ni simu bora kabisa katika soko la smartphones za kishua kwa sasa. Hata hivyo wengine wanasema haina vitu vya kushangaza ili kujitofautisha na zile za mwanzo ama za wapinzani wake husasani simu za kampuni ya Apple.

Samsung ilikuwa na asilimia 30 ya smartphones zote zilizouzwa duniani mwaka jana, karibu mara mbili ya share ya wapinzani wake Apple.

Pamoja na upinzani kutoka kwa Apple, Samsung kwa sasa inakabiliwa na upinzani mkubwa kutoka kwa simu za Huawei za China ambazo huuza simu zake kwa bei chee. Kutokana na changamoto hiyo, bei ya S5 ipo chini kuliko ilivyokuwa S4.
Previous Post Next Post