Askari wa Kenya mwenye shepu iliyowafanya viongozi wake wampige mkwara kutoka na mavazi yake

Huenda ukawa umeshakutana kwenye mitandao ya kijamii na picha ya askari polisi wa Kenya aliyevaa sare (hususan sketi inayobana) zinazolionesha kwa uzuri umbo lake matata.




Trafiki huyo wa kituo cha polisi cha Kiambu, Linda Okello aliitwa na kamanda wa polisi kaunti hiyo James Mugeria na kupewa onyo kali kutokana na uvaaji wake. “Kamanda wa kaunti alimuuta na kumuonya kwa picha hizo zilizosambaa zinazomuonesha akiwa na sketi iliyobana,” alisema afisa mmoja wa polisi.


Ofisa huyo alikuwa kazini na kupigwa picha akiwa na askari mwenzie Kiambu.
Previous Post Next Post

Popular Items