Picha: Lupita Nyongo akiwa na Rihanna kwenye 'The Paris Fashion Week ' Iliyofanyika Nchini Ufaransa

Ni muda wa Lupita Nyongo kushine, Kutokana na umaarufu alioupata Hollywood na dunia kwa ujumla kupitia filamu ya ’12 Years A Slave’ unazidi kumkutanisha na watu mbalimbali maarufu na wakubwa, na safari hii Lupita amekutana na star wa ‘Diamonds’ Rihanna.



Ilikuwa ni katika onesho la mitindo ‘The Paris Fashion Week’ lililofanyika huko Paris jana Jumatano, Ufaransa ndipo mastaa hao walikutana na na kushare muda wao pamoja na mwisho kupiga picha pamoja.






Kupitia Instagram mshindi wa tuzo za Oscar Lupita mwenye miaka 31 alishare moja ya selfie aliyopiga na ‘bad girl’ Riri.

Hivi sasa tunasubiri surprise ya kuja kusikia star wa Hollywood ambaye atabahatika kuiokota almasi (penzi) ya star huyo mzaliwa wa Mexico mwenye asili ya Kenya.





Previous Post Next Post