Nisher afunguka juu ya video mpya ya Shilole, ‘ The EXPLICIT version ni ya Internet tu! ya TV itakua Clean Version’

Director anayeumiza vichwa vya madirector wengi Bongo "Nisher Baby" amefungka na kuwaondoa wasiwasi mashabiki waliocommentvideo hiyo ya shilole kupitia Mtndao wa Youtube, Director Nisher ameachia video hiyo ya shilole inayoitwa Chuna Buzi ikiwa ni video yake ya tatu kw mwaka 2014


Video hiyo ambayo mwanzoni inaanza na onyo la ‘Parental Avasory Explicit Content’ ikimaanisha ndani ina maudhui ambayo yanaweza kuwa hayafai kuonwa na watu fulani mfano watoto, imeonekana kuwapa wasiwasi baadhi ya mashabiki wa kazi za Nisher katika ukurasa wake wa facebook pamoja na Instagram.


Hizi ni baadhi ya comment za Mashabiki Kuhusian na Video ya Shilole 'Chuna BuziThe EXPLICIT version ni ya Internet TU!'





“video kali bro lakini hat hat sana kufungiwa” aliandika mmoja wa watu walio comment.

Hizi ni comments nyingine za watu walioonesha wasiwasi wao wa video hiyo kuchezwa kwenye TV

-Brother nimeiona kali tatizo wabongo wata gomba, kama walivyo ibana y Jux.

-kichupa safi sema kama vile TCRA wanaifungia..very soon..ikipita Amen…lets hope

-unge achia na iyo clean vision ingekuwa pouwa xaaana

Hizo ni baadhi ya comments za wale walioonesha wasiwasi kama video hiyo inaweza kukubalika kuchezwa katika vituo vya runinga hapa bongo, ukizingatia kuwa tayari kuna baadhi ya video ambazo zinasemekana kufungiwa kutokana na kuwa na maudhui ambayo hayafai kwa jamii.

Nisher ametoa ufafanuzi kuwa video ya ‘Chuna Buzi’ iliyoachiwa mtandaoni ni ‘EXPLICIT version’ lakini itakayosambazwa kwenye TV itakuwa safi inayoweza kutazamwa na watu wote.

“The EXPLICIT version ni ya Internet TU! ya TV itakua Clean Version.”Aliandika Nisher katika ukurasa wake wa Facebook.


Baadhi ya video zinazodaiwa kufungiwa kutoka Bongo ni pamoja na ‘Nimevurugwa’ ya Snura, ‘Kabinti Spesho’ ya Dully Sykes na zingine.
Previous Post Next Post