Lil Wayne asema hatatoa 'solo albam' tena baada ya Tha Carter V

Muanzilishi wa Young Money, Lil Wayne amesema baada ya kutoa albam ya ‘Tha Carter V’, hatatoa tena albam kama solo labda ashawishiwe kwa pesa kati ya dola milioni 25 hadi milioni 35.




“Binafsi nimepanga kuwa hii iwe albam yangu binafsi ya mwisho (The Carter V), ndiyo, na itakuwa kweli albam ya mwisho ya Carter. Inaishia kwenye tano.” Weezy aliiambia MTV News.


Habari zaidi kuusu lili wayne bofya hapa

Hata hivyo rapper huyo amesema baada ya kuacha kutoa albam atajikita zaidi katika kufanya albam za pamoja hususani zile anazofanya na kundi la YMCMB.

“Wakati wowote napotaka kufanya kwa ajili ya Young Money, albam ya ‘Like Father, Like Son’ na vitu kama hivyo na labda kitu chochote kinachotokea.” Aliongeza kabla ya kudai kuwa labda mtu ampe dola milioni 25 au 35 kumshawishi abadili mawazo.

Amedai kwa sasa anaweka nguvu zote kwenye mradi wake huo na kwamba hadhani kama atakuja kuwenga nguvu kama hizo kwenye chochote hapo baadae.
Previous Post Next Post