Rapper DMX kuzichapa ulingoni Na George Zimmerman ni katika pambano la raundi 3

George Zimmerman ni Mtu aliyetuhumiwa kuhusika na mauaji ya Mmarekani mwenye asili ya Afrika, Trayvon Martin, mwaka 2012, George Zimmerman, aliyeachiwa huru mwaka jana, atazichapa na rapper DMX kwenye pambano la ndondi la raundi 3, imefahamika.

Endelea kupata Habari Zaidi Kila siku Kutoka BONGO61.COM  Kwa Kijiunga Hapa Buree!.



Walisema haya kila mmoja alipoojiwa.....





DMX
“I am going to beat the living f**k out him … I am breaking every rule in boxing to make sure I f**k him right up,” DMX aliuambia mtandao wa TMZ.

Endelea kupata Habari Zaidi Kila siku Kutoka BONGO61.COM  Kwa Kijiunga Hapa Buree!.

George Zimmerman





Zimmerman ndiye aliyependekeza kuwa na pambano la ngumi na staa yeyote.

Pambano hilo limeandaliwa na promoter maarufu, Damon Feldman wa kampuni ya Celebrity Boxing. Wiki iliyopita alisema alikuwa anakubali ombi la mtu yeyote atakayependa kupanda ulingoni kupambana na Zimmerman katika pambano litakalooneshwa kwa kulipia.

Endelea kupata Habari Zaidi Kila siku Kutoka BONGO61.COM  Kwa Kijiunga Hapa Buree!.

“Habari hiyo ina saa moja tu e-mail yangu imejaa zaidi ya watu 8,000 wanaotaka kuchuana na George, ” Feldman aliiambia CNN wiki iliyopita.

Mapema Jumatano hii amesema amemchagua mshindani. Katika maombi zaidi 15,000 yaliyotumwa kwa e-mail, amesema amemchagua DMX. Tarehe, muda na sehemu ya pambano hilo itatangaza Jumatano ijayo.

Source: Tmz
Previous Post Next Post

Popular Items

WAKUU WA USALAMA KUHOJIWA KENYA