Mpenzi wa Diddy Cassie akanusha tetesi za kuchumbiwa kwenye Instagram

Mpenzi wa rapper na mfanyabiashara P. Diddy aitwaye Cassie Ventura (27) amekanusha tetesi zilizoenea wiki iliyopita kuwa Diddy amemchumbia kupitia Instagram.



Kilichotokea ni kwamba Sean Combs aka Diddy alipost picha ya pete ya almasi katika mtandao wa Instagram na kuandika “Baby do you like it? I just want to get you wat you Like ! I just wanna Mk you smile #takeDat. (sic).”
Baadaye mitandao mbalimbli iliripoti kuwa huenda Diddy amemchumbia mpenzi wake huyo wa muda mrefu japo wengine walihisi ni stunt.

Cassie amevunja ukimya na kuzichimbia shimo tetesi hizo kwa kusema hajachumbiwa.
“I need more, Happy & in love -not engaged,” ameandika Cassie kupitia Instagram.

Hata hivyo mwakilishi wa Diddy alihojiwa exclusively na Mail Online wiki iliyopita naye alikanusha kuwa Diddy hajamchumbia Cassie.

Diddy na Cassie wamekuwa wapenzi toka mwaka 2007.

Previous Post Next Post