Picha: Beyonce Katika Kuwasuprise Mashabiki Wake Aamua Kununua Album yake Mpya Supermarket

Mwanamuziki Beyonce a.k.a Mama Blue Ivvy Ameamua kuwafanyia fans wake suprise ya nguvu Watu waliokuwa wakifanya shopping katika supermarket ya Walmart iliyoko Tewksbury, Marekani jana usiku (Dec 20) walikuwa surprised kumuona superstar Beyonce aliyefika katika supermarket hiyo kufanya shopping ya sikukuu, na kikubwa zaidi alinunua album yake ya mpya ambayo sasa inapatikana katika maduka ya kawaida.

Beyonce akiangalia cd za album yake mpya baada ya kuanza kuuzwa rasmi

Kipenzi cha Jay Z, Queen Bey alishare picha hizo katika ukurasa wake wa facebook na kuandika ‘A little shopping today at Walmart. #BEYONCÉ is available now in store.’
Mwimbaji huyo wa ‘Crazy in love’ ameonekana akinunua nakala ya Cd ya album yake mpya ‘Beyonce’ ambayo tayari imeanza kuuzwa katika CD. ‘Beyonce’ ilitoka rasmi alhamisi iliyopita kwa kushitukiza na kuanzwa kuuzwa kupitia iTunes exclusively kwa muda wa wiki moja.





 Beyonce akilipia CD ya album yake aliyoinunua mara baada ya kuingia rasmi sokoni

Katika shopping hiyo Queen Bey ametumia $37,500 (Milioni 59 Tshs) kwaajili ya manunuzi ya zawadi za Christmas, na kuwazawadia watu waliokuwemo katika supermarket hiyo kadi za X-mas, kila moja ikiwa na thamani ya $50 iliyoandikwa “Happy Holidays from Beyonce.”



Previous Post Next Post

Popular Items